Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema
kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba
Mh.Jaji Joseph Warioba ni sahihi na kwamba kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa
aliyofanyiwa Jaji Warioba ikidaiwa kuongozwa na Paul Makonda, Mzee Sitta
amesema kimsingi wananchi wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa hivyo
hawako tayari kuona akina Warioba wanawapotosha.
Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea
kufanya midahalo ya kupinga Katiba anaweza kuaibishwa kuliko
aliyofanyiwa pale Blue Pearl Hotel.
Pia amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.
Ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo na kukushughulikia. Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta alicheka na kusema hatajibu swali hilo.
Pia amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.
Ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo na kukushughulikia. Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta alicheka na kusema hatajibu swali hilo.